Wednesday, November 3, 2010

Japo ni masikini, Tanzania yaongoza kwa kutoa misamaha ya kodi A. Mashariki





WAKATI serikali ikiendelea kutegemea misaada katika kufanikisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo, imebainika kuwa pato la Taifa linaathiriwa na misamaha mingi ya kodi.

Taarifa ya Taasisi ya Uwazi Twaweza iliyokariri taarifa za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inaonyesha kuwa mwaka wa fedha wa 2009/ 10 pake yake serikali ilitoa miasamaha ya sh 695 bilioni sawa na asilimia 2.3 ya bajeti ya mwaka huo tofauti na Kenya ambayo hutoa misamaha ya asilimia moja tu.

Misamaha hiyo inawanufaisha zaidi wawekezaji wakubwa wenye vyeti vya kupatiwa motisha kutoka katika Kituo cha Uwekezaji Tanzania (Tanzania Investment Centre) na Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (Zanzibar InvestmentPromotion Authority).

Misamaha hiyo hutolewa hasa kwa kuwa Bunge la Jamhuri ya Muungano halipati nafasi sawia ya kupitia matumizi yote ya serikali na hivyo kuifanya kuwa matumizi yaliyofi chika (hidden expenditures).

Taarifa hiyo imetaja mambo tisa, yanayoonyesha upotevu wa fedha za serikali katuika misamaha ya kodi.
Kwanza taarifa hiyo imeonyesha kuwa kiasi kikubwa cha kodi hakikusanywi.

Inasema kuwa, misamaha ya kodi iliongezeka takribani mara mbili ndani ya mwaka mmoja, ikipanda kutoka sh 459 bilioni mwaka 2004/05 hadi sh 772 bilioni mwaka 2005/06. Mwaka 2009/10 misamaha ya kodi ilifikia sh 695 bilioni. Kiasi hicho ni zaidi ya nusu ya sh 1.3 trilioni ambayo Serikali inapanga kukopa kutoka taasisi za fedha za nchi za nje kwa ajili ya kugharimia ujenzi wa miundo mbinu mwaka 2010/11.

“Kama kiasi hiki cha fedha kingekusanywa, kingewezesha rasilimali kwa ajili ya elimu kuongezwa kwa zaidi
ya asilimia 40 au kingefanikisha kupatikana kwa asilimia 72 zaidi ya rasilimali kwa ajili ya afya mwaka 2009/10” inasema taarifa hiyo.

Jambo la pili limeelezwa kuwa Tanzania inatoa misamaha ya kodi zaidi ikilinganishwa na
majirani zake Uganda na Kenya.

“Nchini Tanzania kati ya miaka ya 2005/06 na 2007/08
misamaha ya kodi ilikadiriwa kuwa wastani wa asilimia 3.9 ya pato la taifa. Mwaka 2008/09 misamaha ya kodi ilikuwa asilimia 2.8 ya pato la taifa na mwaka 2009/10
asilimia 2.3. Ukilinganisha na Kenya na Uganda misamaha ilifikia asilimia 1 na 0.4 ya pato
la taifa la kila nchi husika4 kwa mtiririko huo.

Jambo la tatu, imebainishwa uwa chini ya utawala wa Rais Kikwete misamaha ya kodi imeongezeka kwa kasi,
“Katika kipindi cha miaka mitano (2006-2010) ya Rais Kikwete, misamaha ya kodi ilikuwa
asilimia 1 ya pato la taifa (au asilimia 40) zaidi ya misamaha iliyotolewa wakati wa kipindi
cha pili cha uongozi wa Rais Mkapa (2001-2005).

Jambo la nne limebainisha kuwa wawekezaji wakubwa wa kimataifa wananufaika zaidi na
misamaha ya kodi.

Kwa mujibu wa ripoti ya mapato ya kodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inaonesha kuwa makundi matatu yanapata misamaha mingi zaidi.
Haya ni makampuni yenye vyeti vya kupatiwa motisha vinavyotolewa chini ya Sheria yaUwekezaji Tanzania na Sheria ya Kuendeleza na Kulinda Uwekezaji Zanzibar,
walipaji wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) chini ya vifungu na 220, 223 na 224; na makampuni ya madini chini ya Sheria ya Madini.

Jambo la tano kwa mujibuwa ripiti hiyo, misamaha kwa bidhaa kutoka nje inachukua asilimia 75 ya
misamaha yote.

“Misamaha ya kodi inayotolewa kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inaweza kuwekwa katika makundi makuu mawili: Misamaha inayohusiana na uagizaji wa bidhaa nje ya nchi (ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa) na misamaha inayotolewa chini
ya vipengele vya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT). Katika miaka miwili iliyopita,
sehemu kubwa ya misamaha ya kodi iliyotolewa ilihusisha ushuru wa forodha na ushuru
wa bidhaa zinazoagizwa toka nje ya nchi.”
Jambo la sita, inaonyesha kuwa Zanzibar inatoa mara mbili ya misamaha ukilinganisha na Bara.

Misamaha ya kodi inatolewa pande zote mbili za Muungano, hata hivyo, kama sehemu ya mapato, misamaha ya kodi imeongezeka kwa kasi zaidi
Zanzibar.

“Katika kipindi cha 2006-2010, misamaha ya kodi iliyotolewa na Mamlaka ya
Mapato (TRA) upande wa Zanzibar ilikuwa karibu asilimia 46 ya mapato yaliyokusanywa
ukilinganisha na asilimia 26 katika kipindi cha 2001-2005.

Hata hivyo taarifa hiyo inaonyesha kuwa misamaha ya kodi imeanza kupungua ambapo Serikali kupitia Wizara ya Fedha imeonesha dhamira hiyo.

“ Kwa hakika misamaha ya kodi imeshuka kutoka kilele cha TZS 840 bilioni (au
asilimia 4.3 ya pato la taifa) mwaka 2006/07 hadi TZS 695 bilioni au asilimia 2.3 ya pato
la taifa mwaka 2009/10. Japokuwa haya ni maendeleo chanya, ikiwa katika kiwango
cha asilimia 2.3 ya pato la taifa misamaha ya kodi inayotolewa na Tanzania imeendelea
kubakia kuwa zaidi ya kati ya mara 2 na 6 ya ile ya Kenya na Uganda.”

Lakini taarifa hiyo inabainisha kuwa japo misamaha kwa mashirika yasiyo ya kiserikali na wawekezaji wakubwa imepungua, imeongezeka kwa miradi ya wafadhili na taasisi za Serikali.

“Kati ya mwaka 2008/09 na 2009/10 kiwango cha misamaha iliyotolewa kilipungua kutoka
TZS 752 bilioni hadi TZS 695 bilioni”.

Kwa kuwa Misamaha ya kodi ni upendeleo uliopitishwa kisheria inakuwa vigumu kuiondoa kama imeshawekwa. Hii inamaanisha kuwa kabla misamaha haijaruhusiwa kutolewa, sheria inahitajika kuainisha ni aina gani ya watu, mashirika ama bidhaa zisamehewe kodi.

“Mara sheria inapopitishwa na kuanza kutekelezwa ni vigumu kuuondoa upendeleo huu kwani wahusika wanaweza kutoa hoja za ushawishi ili ziendelee kuwepo. Jitihada za kuondoa misamaha ya kodi zilizofanywa
na Serikali ya Tanzania hivi karibuni zimeonesha ni jinsi gani kuna ugumu katika kuondoa misamaha ya kodi iliyokwisha pitishwa kisheria”

Sunday, October 24, 2010

DK SLAA ITV

Mengi yamesemwa kuhusu mahojiano ya Dk Slaa na ITV. Lakini mimi niliyeshuhudia mahojiano hayo, kwakweli nampongeza Dk Slaa kwa uwezo wake kujibu maswali.

Wanaosema hakusema kitu, mbona wamemkimbiza mgombea wao kwenye midahalo?

Thursday, October 14, 2010

MWAKA HUU, TANZANIA YOTE KWA YESU

Hili ni kanisa la Tanzania Assemblies of God la wilaya ya Namtumbo mkoa wa Ruvuma. Niliipata picha hii nikiwa napita tu njiani sikufanikiwa kuingia ndani kutokana na muda wangu. Inatia moyo.

Wednesday, October 13, 2010

KIKUBWA PUMZI


Joshua Lwendo akimvisha pete ya uchumba Happy Sasali katika kanisa la TAG kigogo hivi karibuni. Nasikia ndoa yao itakuwa December. Hapo Joshua anaingia kwenye majukumu kama baba, kaza msuli, kikubwa pumzi tu.

CHAGUENI HIVI LEO MTATUMTUMIKIA NANI?


Hao ni CFF wakiperform siku ya sikukuu yao pale TAG Kigogo hivi karibuni

HAPA WANASAJILI WASANII WA TUSKER PRPJECT FAME


Tuesday, September 28, 2010

MAMBO YA NAIROBI


ELIFADHILI NA CATHERINE WANG'ARA


Ilikuwa heka heka nguo kuchanika pale Elifadhili na Catherine walipofunga ndoa katika kanisa la TAG Kigogo na tafrija ya kukata na shoka iliyofanyika katika ukumbi wa CASSA Mikocheni Dar es Salaam.











Monday, September 20, 2010

BARAKA YA MTOTO

Namshukuru Mungu kwa kutupatia mtoto wa kiume wa pili. Jina lake ataitwa Solomon.
Pichani Solomon akiwa amebebwa na kaka yake, Gibson.

MUZIKI WA CUF MIKOA YA KUSINI

Picha hizi zinaonyesha wafuasi wa Chama cha wananchi CUF wakifurahia mikutano ya mgombea urais wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba.










Meno 32 nje



Monday, August 23, 2010

KAMPENI NDIYO HIZO ZIMEANZA

Kama ilivyo katijka machezo, wote husindana lakini atakayepata ni mmoja tu. Hao Ni CCM, CUF na Chadema. Nani atachukua urais.





Monday, August 16, 2010

Thursday, August 5, 2010

STELLA'S SEND OFF, ILIKUWA BOMBA KWELI KWELI











KEKI YA BIRTHDAY


Kama mmezoea kukata keki kubwa zenye ngazi, mjue hayo yamepitwa na wakati, hiyo ndiyo keki ya kisasa.
Msanifu mkuu wa gazeti la Mwananchi Angetile Osia akikata keki ya birthday yake, kushoto kwake ni mwandishi wa habari za burudani, Julieth Kulangwa.

HUYU NI BABA WA MTU JAMANI

Tangu alipopata mtoto na kutangaza nia ya kuoa nimekuwa nikimshauri apunguze utundu lakini hasikii, basi nawaachia nyie.

Tuesday, August 3, 2010

KURA YA MAONI ZANIBAR



Kura ya maoni kwaajili ya kuamua serikali ya mseto imepokelewa kwa mikono miwili na Wazanzibari hasa Wapemba.



KANISA LAZIDI KUSHAMIRI PEMBA

Baadhi ya washirika wa kanisa la TAG Chakechake Pemba wakiwa kwenye ibada hivi karibuni.
Kwa sasa kanisa hilo linakua kwa kasi kisiwani humo ambako idadi ya wakazi wake wengi ni waislamu.




Tuesday, July 20, 2010

CHEKI JINSI AL SHABAB WALIVYO
















BAADA ya kundi la waasi nchini Somalia, Al-Shabab lenye uhusiano na mtandao wa Al Qaida kudai kuhusika na mashambulizi nchini Uganda, sasa limeahidi kuendeleza mashambulizi hayo.
Kiongozi wa kundi hilo, Muhammad Abdi Godane amedai kuhusika na mashambulizi ya mabomu yaliyotokea nchini Uganda hivi karibuni na kusema anapanga mashambulizi zaidi.
Kiongozi wa kundi la waasi wa al Shabaab nchini Somalia ametishia kuendeleza mashambulizi ya kundi hilo nchini Uganda katika siku zijazo. ametoa taarifa hiyo kupitia vituo vya redio mjini Mogadishu na kusisitiza kuwa, kile kilichojiri hivi karibuni mjini Kampala ni mwanzo tu.
“Tutaendelea kukabiliana na maadui wa nje popote walipo. Hakuna atakayetuzuia kutekeleza kazi zetu za kiislamu” anasema Sheik Ali Mohamud Rage, msemaji wa kunpdi hilo mjini Mogadishu.
Mabomu ya Jumapili yameua zaidi ya watu 70 waliokuwa wakiangalia fainali za kombe la dunia kwenye televisheni mjini Kampala.
Kati ya waliouawa ni mfanyakazi wa kutoa misaada wa Marekani pia ameuawa. Wanachama wengine sita wa kanisa kutoka Pennsylvania Marekani walijeruhiwa vibaya katika mlipuko huo uliolengwa nje ya uwanja wa mkahawa wa Kiethiopia mjini Kampala.
Damu na viungo vya binadamu vilikuwa vimetapakaa sakafuni na kwenye viti vilivyopinduliwa na mlipuko huo wakati watu walipiokuwa wakiangalia mechi kati ya Hispania na Uholanzi.
Kamanda wa jeshi la Al-Shabab Yusuf Sheik Issa amefurahia tukio hilo la kwanza kufanywa na kundi hilo nje ya mipaka ya Somalia.
"Uganda ni moja ya maadui zetu, kila kinachowaliza kinatupa furaha. Tunaomba hasira za Allah's ziwe juu ya wote walio kinyume na sisi” anasema Sheikh Issa.
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni ameapa kujibu vikali. Amesema wanajeshi wa Uganda nchini Somalia wanashughulikia ulinzi, lakini wataanza kulivunja kundi la Al Shabab.

Thursday, July 1, 2010

WABONGO NA KUSAJILI LINE ZA SIMU

Walipotangaza kuongeza muda, watu wakawa hawaendi. siku zilipokaribia kwisha ndiyo wanajazana. Siku zimeongezwa tena, hukuti mtu kwenye usajili, wanasubiri siku za mwisho.

Hata sasa hivi watu wakiambiwa kuwa Yesu atarudi mara ya pili, hawaamini kabisa. Sasa tofauti yake ni kwamba, kwa Mungu hakutakuwa na muda wa nyongeza wa kutubu.








Tuesday, June 29, 2010

SUGU KUGOMBEA UBUNGE KWA TIKETI YA CHADEMA


Yule mwasisi wa Muziki wa Bongo flavour, Joseph Mbilinyi aka Mr II au ukipenda mwite Two Proud au hata Sugu, sasa ametangaza nia ya kugombea Ubunge katika jimbo la Mbeya Mjini kwa tiketi ya Chadema.

Uamuzi wa mshikaji umekuja siku chache tu tangu alipotiwa mbaroni na jeshi la polisi akidaiwa kutoa wimbo wenye maudhui ya kumtishia kifo Mkurugenzi wa Clouds entertainment, Ruge Mutahaba.

Hata hivyo yeye amekanusha madai hayo akisema kuwa maneno yaliyomo katika wimbo wake huo hasa lile la 'Kill' hayamaanishi kuua bali kuondoa.

Mwenyewe anakichukulia kitendo hicho kama fitna anazofanyiwa na wabaya wake katika kufanikisha malengo yake mbele ya Watanzania.

"Mimi niko katika mapambano, hata kama kesi hizi zitanipeleka jela, basi ndiyo itakuwa mwisho wangu, lakini sijakata tamaa" alisema Sugu katika mahojiano naye tuliyoyafanyia Sinza Jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Saturday, June 26, 2010

JAMAA KACHOKA KUISHI, AU ANATAKA KUVUNJA REKODI YA GUINESS?

Kijana mmoja ambaye hakujulikana mara moja akiwa juu ya nguzo ya umeme wenye nguvu kubwa maeneo ya Ubungo. Sijui amechoka maisha au anataka kuweka rekodi!






Wananchi wakimwangalia kijana huyo kwa makini.























Friday, June 25, 2010

THE BEST GROUP

When I completed my university exams at Msimbazi Centre Dar es Salaam on 18, June 2010. From left, Neema Laizer, Elias Msuya, Nyanzala Kwelukwa, Elizabeth Kilato and Frank Sendwa.


Monday, June 21, 2010

MGOMBEA BINAFSI IMEKUWA ISSUE


Mahakama ya rufani imechakachua demokrasia

Elias Msuya

HUKUMU iliyotolewa hivi karibuni na Mahakama ya Rufani nchini kuhusu kesi ya mgombea binafsi, ina utata mkubwa. kama tulivyozoea kusikia mafuta ya dizeli na petroli yakichakachuliwa na mafuta ya taa, basi mahakama hiyo nayo sasa imechakachua demokrasia.

Katika hukumu hiyo, Mahakama hiyo imesema kuwa sulala la mgombea binafsi siyo la kisiasa bali ni la kisiasa hivyo linapaswa kupelekwa Bungeni ili lijadiliwe na kutolewa uamuzi.

Itakumbukwa kuwa shauri hili lilifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza na Mchungaji Mtikila katika Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma na Mahakama hiyo kupitia kwa Jaji Kahwa Lugakingira, ikaruhusu mgombea binafsi mara baada ya vyama vingi kuanza mwaka 1992. Baada ya Serikali kubwagwa, ilikwenda bungeni na kufanya marekebisho ya sheria na kuvifanya vifungu vilivyotajwa na Mahakama kuwa vinatoa fursa ya kuwapo mgombea binafsi, vikaondolewa na kutamka kuwa mtu anaruhusiwa kugombea kupitia vyama vya siasa. Baada ya marekebisho hayo, Mtikila alifungua tena kesi Mahakama Kuu kwa maelezo kuwa marekebisho hayo yanakiuka haki za binadamu na yako kinyume cha Katiba. Safari hiyo jopo la majaji watatu chini ya Jaji Kiongozi Amir Manento likatamka kuwa vifungu vilivyorekebishwa na Bunge vinakiuka Katiba yenyewe. Majaji hao wakaenda mbali zaidi na kumwagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuandaa mazingira kuanzia hukumu hiyo ilipotolewa hadi uchaguzi wa Oktoba kuwe na sheria inayoruhusu mgombea binafsi. Baada ya hukumu hiyo, Serikali haikuridhika ikakata rufani ambayo sasa ndiyo imetolewa huku hivi karibuni kuwa suala hilo si la kuamuliwa na Mahakama, bali Bunge.

Wasiwasi wangu ni kwamba, kwakuwa suala hili limerudishwa Bungeni, serikali italitumia Bunge kama mhuri kuizika kabisa hoja hii. Kwa kuwa Bunge letu limetawaliwa na wabunge wa CCM, ni wazi kuwa wataipinga tu hoja hiyo na ndiyo utakuwa mwisho wake.

Mimi siyo mwanasheria kitaaluma, lakini nashawishika kuona kwamba mahakama ya rufani imekwepa jukumu lake la kisheria na kuliita kuwa la kisiasa.

Ikumbukwe kwamba, madai ya Mchungaji Mtikila yanatokana na Katiba. Anadai kuwa sheria inayokataza mgombea binafsi inapingana na Katiba ibara ya 21 (1) na (2) . Kwa hiyo kinachotakiwa hapa siyo kubadilisha katiba bali ni kuitafsiri Katiba inayotoa haki ya kila raia kuwa huru kushiriki siasa bila kujiunga na chama au kundi fulani.

Katiba ni sheria na kazi ya mahakama ni kutafsiri sheria, hivyo ilipaswa kuitafsiri sheria hiyo kama ilivyoanya kwenye hukumu za awali.

Suala la mgombea binafsi ni haki ya binadamu, ni hali inayotambuliwa na Katiba. Inashangaza kuona serikali yetu inayosema kuwa inafuata misingi ya haki za binadamu ikikiuka haki hii.

Hata tafiti mbalimbali zilizofanywa hapa nchini zimebaini kuwa, Watanzania wengi wanataka haki ya kuwa na mgombea binafsi.

Mfano ni ripoti ya Mchakato wa kujipima kwakutumia utawala bora (APRM) iliyotoka mwaka huu, imebainisha kuwa Watanzania wengi wanataka haki ya kuwa na mgombea binafsi.

Kwa hiyo kwa kuzingatia utamaduni na siasa za nchi yetu, hili nalo lingepasw kuangaliwa.

Ukweli ni kwamba CCM inaiogopa hoja ya mgombea binafsi kwani inaweza kuisambaratisha kabisa. Usione watu wengi wakati huu wa uchaguzi mkuu wakitangaza nia ya kugombea uongozi kwa tiketi ya CCM. Hawana jinsi, maana ukitaka kufanikiwa kirahisi, sharti ujiunge na CCM.

CCM imejilimbikizia ushindi kiasi kwamba mtu akienda kugombea kwa vyama vya upinzani inambdi awe na moyo wa jiwe.

Wanajua kama sheria ya mgombea binafsi ikipitishwa watu wengi maarufu ndani ya chama hicho watakimbia na kugombea kama wagombea binafsi.

Kuna hoja mbalimbali zinasemwa na wanaopinga sheria ya mgombea binafsi. wapo wanaosema kuwa sheria hiyo ikiruhusiwa, kutatokea machafuko, wengine wanahoji, mgombea binafsi atakuwa akidhibitiwa na nani kinidhamu?

Lakini tukumbuke kwamba sheria hiyo ingepitishwa, basi ingeweka miongozo ya kuwadhibiti wagombea binafsi hata wanaposhinda chaguzi.

Huu ni woga wa bure tu kwa serikali kwasababu, zipo nchi kama Marekani, zimeruhusu wagombea binafsi, lakini hakuna athari yoyote. Kibaya zaidi hata wagombea binafsi wanaposimama kugombea wala hawafahamiki kama wale walioko kwenye vyama vikubwa vya Republican na Democratic achilia mbali vyama vingine.

Tukumbuke pia kwamba vyama vya siasa vimekuwa kikwazo kikubwa cha demokrasia hasa kwakuwa vimekuwa kama kampuni za watu Fulani wanaojiona kuwa wamiliki wa vyama hivyo.

Hata kama mgombea anakubalika kwa wananchi, kama “wenye chama” hawamtaki basi hapiti. Huko ni kuchakachua demokrasia. Demokrasia ni uhuru wa watu kuchagua kiongozi wanayemtaka, siyo kuamuliwa na chama wamchague nani.

Mahakama ambayo ndiyo chombo cha kutoa haki kwa wananchi ilipaswa kusimama kidete kupigania haki hii kama ilivyokuwa imefanya mwanzo.

Lakini kwa kitendo hiki, wananchi wameachwa solemba na hawajui tena kama kuna chombo kingine kitakachotutetea katika kupigania haki zao.

Changamoto nyingine inayojitokeza ni marekebisho ya katiba yetu. Wataalamu wengi na wadau wa sherai wamekuwa wakitoa wito wa kurekebishwa kwa Katiba yetu, lakini serikali imekuwa ikipinga.

Matokeo yake sasa Katiba imekuwa ikijichanganya yenyewe kwa kuwa na vifungu vinavyopingana hivyo kuwa na mvurugano katika utawala na wananchi.

Huku ni kuchakachua demokrasia. Demokrasia ambayo tumeiridhia tunaichanganya na matakwa ya watawala wachache wenye lengo la kutawala milele nchi hii.

Elias Msuya ni mwandishi wa makala wa Gazeti la Mwananchi 0754 897 287





Monday, June 14, 2010

YAMETIMIA

Ilikuwa ni siku ya furaha kweli kweli pale Kabora na Naomi walipofunga pingu za maisha jijini Dar es Salaam.




Monday, May 17, 2010

KABORA ANG'ARA


Mchungaji Elisa Kabora akimvisha pete ya uchumba Naomi katika kanisa la TAG Kigogo mjini Dar es Salaam hivi karibuni.

MJOMBA


Camera yetu ilimnasa Mrisho Mpoto akisherehesha siku ya Meimosi.

MAMBO YA ARUSHA

Wale waliokuwa wakisema kuwa "Utamaliza kuni kwa kuchemsha mawe" wamechemsha. Soma hii........ (Mawe yameiva, kuni zimebaki)
















Huyu mwendesha mkokoteni au bepari?


Hapo ndiyo Arusha
Huu mnara sasa umeshapoteza maana yake kwani wakazi wa Arusha sasa wanautumia kupigia picha za video, hawakumbuki tena lile Azimio la Arusha.