Wednesday, September 30, 2009

HUYU NDIYE DK SALIM AHMED SALIM







Dk Salim: WanaCCM waachwe
wapambane na Kikwete 2010

ASEMA MFUMO WA SERIKALI UMEOZA KWA RUSHWA

Elias Msuya

MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM na waziri mkuu wa zamani, Dk Salim Ahmed Salim amesema kuwa wanachama wa chama hicho wanaotaka kugombea urais sambamba na Jakaya Kikwete waachwe wapambane naye, lakini akasema hawatamuweza.

Baadhi ya jumuiya za CCM na vikundi kadhaa ndani ya chama hicho vimeshamtangaza Kikwete kuwa mwanachama mwingine asijitokeze kupambana na Kikwete kwenye uchaguzi ujao na kwamba vinamuunga mkono kiongozi huyo.

Lakini Dk Salim, ambaye aliwahi kuwa katibu mkuu wa Umoja wa Afrika (OAU), aliiambia Mwananchi katika mahojiano maalum nyumbani kwake jijini Dar es Salaam jana, WanaCCM wana haki ya kupambana naye kuwania kuteuliwa kugombea urais kwa tiketi ya chama hicho tawala..

Dk Salim alisema si makosa kwa wanachma wa CCM kujitokeza kuomba ridhaa ya wanachama kugombea urais kwa tiketi ya CCM katika kipindi cha kwanza cha rais aliye madarakani.

Alisema kwamba licha ya kuwepo kwa utaratibu wa CCM wa kumuachia rais aliye madarakani amalizie vipindi viwili vya madaraka yake, bado haoni tatizo kwa mwanachama wa chama hicho kujitokeza kugombea urais.

Alisema kwamba hata kama wanachama hao watajitokeza watapitia kwenye taratibu na mchakato wa chama wa kuwachuja.

"Huo ni utaratibu wa CCM ambao una maslahi kwa chama. Hata hivyo, watu wanaweza kujitokeza tu kugombea sambamba na Rais Kikwete. Kama watajitokeza watapitia kwenye mchakato wa chama ambacho ndicho kitaamua kimpitishe nani. Hata hivyo, kwa sasa sioni mtu wa kumshinda Rais Kikwete," Dk Salim alisema.

“CCM ina utaratibu wa kuachiana vipindi viwili. Ni utaratibu uliowekwa kwa maslahi ya chama katika mazingira ya siasa za leo. Lakini, hata kama watajiotokeza wanachama wengine, bado Rais Kikwete ana nguvu ya kuwashinda. Sidhani kama kuna mwanachama ambaye anaweza kupitishwa zaidi ya Kikwete,”.

Hadi sasa mbunge wa jimbo la Maswa mkoani Shinyanga, John Shibuda ndiye pekee aliyetangaza nia yake ya kuvaana na Kikwete kuomba ridhaa ya chama kugombea urais katika uchaguzi wa mwaka 2010.

Makamu mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa alishaweka wazi kwamba katika mchakato wa kumpata mgombea urais kupitia chama hicho mwakani ni ruksa kwa wanachama kuomba nafasi ya urais kwa kuwa katiba inawaruhusu.

Lakini kabla ya Msekwa kutoa ufafanuzi huo, makamu mwenyekiti wa zamani wa CCM, John Samuel Malecela, kundi la wenyeviti wa mikoa na wazee wa chama hicho, walitangaza wazi kwamba Rais Kikwete apitishwe amalizie kipindi chake cha pili cha uongozi kama ilivyo desturi ya chama hicho.

Mfumo wa serikali unanuka rushwa

Akizungumzia suala la mapambano ya rushwa, Dk Salim alisema mfumo wa serikali ya Tanzania umeoza kwa rushwa na hivyo hauwezi kumsaidia rais kuikabili, hivyo rushwa kutawala kuliko kitu kingine.

Alisema tofauti na wakati wa rais wa awamu ya kwanza, Mwalimu Julius Nyerere wakati rushwa ilipodhibitiwa kikamilifu, wakati huu rushwa imeachiwa nafasi kubwa kiasi ambacho kinafanya hali ya Watanzania kudorora.

“Tukisema kwamba tatizo halipo tutakuwa tunakosea. Tulilokosea ni kuliachia tatizo la rushwa lishamiri kama lilivyoshamiri sasa. Rushwa haikuanza jana, haikuanza na serikali ya awamu ya nne, wala serikali ya awamu ya tatu wala ya pili. Rushwa ilikuwepo tangu awamu ya kwanza," alisema.

Lakini akasema tofauti kubwa kati ya awamu hizo na ile ya Mwalimu Nyerere ni kwamba muasisi huyo wa taifa alionyesha kwa vitendo kuwa rushwa ni jambo aliloamua kulifungia mkanda na kupambana nalo, lakini baada ya hapo tatizo hilo limeachiwa liendelee kiasi cha rushwa kugeuka kuwa utaratibu.

Alisema kwamba licha ya nia njema ya Rais Kikwete ya kupambana na rushwa na ufisadi, bado mfumo mzima wa serikali umeoza kiasi ambacho haiwezekani kupambana na rushwa.

“Rais Kikwete anajitahidi na ana nia ya kupambana na rushwa, lakini bado 'system' (mfumo) haijajitayarisha vya kutosha kupambana rushwa,” alisema.

Licha ya kuitetea CCM kuwa haihusiki na ufisadi bali baadhi ya watendaji wake ndiyo wanaojihusisha na ufisadi, Dk Salim alisema rushwa ni kansa inayoitafuna nchi.

“CCM kama chama si tatizo bali baadhi ya viongozi hawafuati katiba ya chama. Rushwa ni kansa inayoathiri jamii ya Watanzania. Mategemeo ya wananchi ni kuona CCM ndiyo iwe mstari wa mbele kupambana na rushwa na ufisadi kwa sababu hata katiba na ahadi za chama zinasema rushwa ni adui, sitapokea wala kutoa rushwa. Sasa hapa ndiyo kwenye tatizo,” alisema Salim.

Aupongeza uongozi wa Spika Sitta

Dk Salim alisema kwamba Bunge la sasa limepiga hatua kubwa katika kutoa kero za wananchi hasa kipindi hiki cha mfumo wa vyama vingi.

“Kwa kweli Spika Samuel Sitta amejitahidi sana kuendesha Bunge lenye viwango, hasa wakati huu wa mfumo wa vyama vingi. Bunge ndiyo sauti ya wananchi; ni njia pekee ya wananchi kutoa kero zao kwa serikali. Kwa hiyo linatakiwa liendeshwe katika 'health environment' (mazingira mazuri),” alisema.
“Tukiwa na Bunge kama hili ambalo linawapa wabunge nafasi ya kuzungumza kama hivi ni safi kwani inakuwa changamoto kwa mawaziri. Inawalazimu mawaziri kuwa na 'home work '(kazi ya ziada) kila wanapokwenda bungeni kujibu maswali" alisema Salim.

Tuesday, September 22, 2009

Pastor and Son

Every Sunday afternoon, after the morning service at the church, the Pastor and his eleven year old son would go out into their town and hand out Gospel Tracts. This particular Sunday afternoon, as it came time for the Pastor and his son to go to the streets with their tracts, it was very cold outside, as well as pouring rain. The boy bundled up in his warmest and driest clothes and said, 'OK, dad, I'm ready.' His Pastor dad asked, 'Ready for what?' 'Dad, it's time we gather our tracts together and go out.' Dad responds, 'Son, it's very cold outside and it's pouring rain.' The boy gives his dad a surprised look, asking, 'But Dad, aren't people still going to Hell, even though it's raining?' Dad answers, 'Son, I am not going out in this weather.'

Despondently, the boy asks, 'Dad, can I go? Please?' His father hesitated for a moment then said, 'Son, you can go. Here are the tracts, be careful son.' 'Thanks Dad!' And with that, he was off and out into the rain. This eleven year old boy walked the streets of the town going door to door and handing everybody he met in the street a Gospel Tract . After two hours of walking in the rain, he was soaking, bone-chilled wet and down to his VERY LAST TRACT.

He stopped on a corner and looked for someone to hand a tract to, but the streets were totally deserted. Then he turned toward the first home he saw and started up the sidewalk to the front door and rang the door bell. He rang the bell, but nobody answered. He rang it again and again, but still no one answered. He waited but still no answer. Finally, this eleven year old trooper turned to leave, but something stopped him. Again, he turned to the door and rang the bell and knocked loudly on the door with his fist. He waited, something holding him there on the front porch! He rang again and this time the door slowly opened. Standing in the doorway was a very sad-looking elderly lady. She softly asked, 'What can I do for you, son?' With radiant eyes and a smile that lit up her world, this little boy said, 'Ma'am, I'm sorry if I disturbed you, but I just want to tell you that * JESUS REALLY DOES LOVE YOU * and I came to give you my very last Gospel Tract which will tell you all about JESUS and His great LOVE.' With that, he handed her his last tract and turned to leave. She called to him as he departed. 'Thank you, son! And God Bless You!'
Well, the following Sunday morning in church Pastor Dad was in the pulpit. As the service began, he asked, 'Does anybody have testimony or want to say anything?' Slowly, in the back row of the church, an elderly lady stood to her feet. As she began to speak, a look of glorious radiance came from her face, 'No one in this church knows me. I've never been here before. You see, before last Sunday I was not a Christian. My husband passed on some time ago, leaving me totally alone in this world. Last Sunday, being a particularly cold and rainy day, it was even more so in my heart that I came to the end of the line where I no longer had any hope or will to live. So I took a rope and a chair and ascended the stairway into the attic of my home.

I fastened the rope securely to a rafter in the roof, then stood on the chair and fastened the other end of the rope around my neck. Standing on that chair, so lonely and broken-hearted I was about to leap off, when suddenly the loud ringing of my doorbell downstairs startled me. I thought, 'I'll wait a minute, and whoever it is will go away.' I waited and waited, but the ringing doorbell seemed to get louder and more insistent, and then the person ringing also started knocking loudly... I thought to myself again, 'Who on earth could this be? Nobody ever rings my bell or comes to see me.' I loosened the rope from my neck and started for the front door, all the while the bell rang louder and louder. When I opened the door and looked I could hardly believe my eyes, for there on my front porch was the most radiant and angelic little boy I had ever seen in my life. His SMILE, oh, I could never describe it to you!

The words that came from his mouth caused my heart that had long been dead, TO LEAP TO LIFE as he exclaimed with a cherub-like voice, 'Ma'am, I just came to tell you that JESUS REALLY DOES LOVE YOU .' Then he gave me this Gospel Tract that I now hold in my hand. As the little angel disappeared back out into the cold and rain, I closed my door and read slowly every word of this Gospel Tract. Then I went up to my attic to get my rope and chair. I wouldn't be needing them any more. You see-- -I am now a Happy Child of the KING. Since the address of your church was on the back of this Gospel Tract, I have come here to personally say THANK YOU to God's little angel who came just in the nick of time and by so doing, spared my soul from an eternity in hell.' There was not a dry eye in the church.

And as shouts of praise and honour to THE KING resounded off the very rafters of the building, Pastor Dad descended from the pulpit to the front pew where the little angel was seated.... He took his son in his arms and sobbed uncontrollably. Probably no church has had a more glorious moment, and probably this universe has never seen a Papa that was more filled with love & honour for his son... Except for One.

Monday, September 21, 2009

Mzee wetu Kawawa


Hivi karibuni nimefanya mahojiano na Mzee Rashid Kawawa kuhusu masuala mbali mbali yahusuyo siasa za Tanzania. Nitawaletea mahojiano hayo muda si mrefu.

Thursday, September 10, 2009

GARI LINAKODISHWA






HI WAPENDWA! GARI YA SHUGHULI! GARI YA SHUGHULI!GARI YA SHUGHULI HII HAPA; (SEE ATTACHMENT), NI GARI YA KISASA KABISA YENYE MBWEDO (CONRFOTABLENESS) WA HALI YA JUU, TUNABEBA MAHARUSI,SEND OFF PARTIES, KITCHEN PARTIES, KOMUNIO, UBATIZO NA VIPAIMARA. GHARAMA ZETU NI ZA CHINI MNO,HUTASHINDWA KUZIMUDU, TUNAJALI MUDA NA UNYETI WA SHUGHULI YAKO, TUPO ILI KUWEZESHA SHUGHULI YAKO, WALIOWAHI KUITUMIA HAWAJAJUTA! WASILIANA NASI KWA NAMBARI ZA SIMU HIZI; 0784 587 905 AU 0655 587 905 AU 0784 494 906 AU 0718 817 706 AU 0754 897 287 KARIBUNI NYOOTE ELIFADHILI S. MSUYA

Kikwete mshikaji kweli!

Mtindo mpya aliouanzisha Rais Kikwete wa kuzungumza na wanananchi kupitia vyombo vya habari ambapo sasa wananchi wana fursa ya kupiga simu, kutuma sms na hata e mail, umeonyesha jinsi ambavyo Rais Kikwete yuko karibu na wananchi kinoma.

Rais Kikwete alisema kwamba amegundua kwamba hata hotuba anazozitoa anapokuwa ziarani huwa haziendani kabisa na matakwa ya wananchi, kwahiyo ni bora tu awape nafasi waulize wanachotaka. Tena Kikwete anataka hata wananchi wawe wanakwenda ikulu wanapokuwa na shida,
"Wakati mwingine ninapokuwa Ikulu huwa nawauliza wasaidizi wangu, hivi hakuna wananchi wenye matatizo wanaokuja hapa Ikulu?" aliuliza Rais Kikwete.

Kufuatia hali hiyo Rais Kikwete amepanga kuwa anakutana na wananchi wenye matatizo nje ya Ikulu kama alivyokuw akifanya Mzee ruksa enzi zile.

Monday, September 7, 2009

Friday, September 4, 2009

Chadema Hooray!

Mwenyekiti wa Chadema freeman Mbowe akipongezwa na wanachama wa chama hicho baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa kiti hicho.

















MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), Freeman Mbowe amefanikiwa kutetea nafasi hiyo kwa mara ya pili baada ya kupata ushindi wakura za ndiyo kwa ailimia 92.9 kutoka kwa wajumbe wa mkutano mkuu uliofanyika jana katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi huo, ambaye pia ni mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, Bob Makani alisema kwamba, kura za hapana kwa nafasi hiyo zilikuwa 22 sawa na asilimia 4.8 wakati kura za ndiyo zilikuwa 425 sawa na asilimia 92.9 na kuongeza kuwa kura zilizoharibika ni 10 sawa na asilimia 2.1.


Baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, ukumbi ulilipuka kwa shangwe na furaha huku baadhi ya wajumbe wakimvamia Mbowe na kumbeba juu juu mpaka katika meza kuu.

Tuesday, September 1, 2009

Maadhimisho ya miaka 45 JWTZ

Eti huyu naye ni mwanajeshi!




Luteni Rose katila, mwanamke pekee anayeendesha ndege za kivita


Waziri wa ulinzi akiwa na baadhi ya maofisa wa jeshi la ulinzi. Nyuma yake ni Mkuu wa majeshi mstaafu, Robert Mboma.





Wananchi waliotembelea maonesho ya JWTZ wakiangalia ndege ye kivita.

Sikukuu ya kwaya TAG Kigogo

Baadhi ya Washirika wakimpa pole Mchungaji Gordon Lwendo nyumbani kwake Mburahati Dar es Salaam.



Soloist, Jane James akighani mashairi ya wimbo mojawapo wa kwaya kanisani hapo.


Rose Mgaya (Mama Uhu) akiwajibika jukwaani





Wanakwaya TAG Kigogo.