Thursday, June 30, 2011

KWANINI WABUNGE WANALALA SANA BUNGENI?

Tatizo lilianza pale wabunge walipoamua kuhamishia ukumbi wao kutoka Karimjee na kwenda Dodoma ambako walijengewa ukumbi wa Msekwa. Ukumbi wa Msekwa ulikuwa wa kifahari kuliko wa Karimjee. kama hiyo haitoshi wakajenga mwingine wa kifahari zaidi wanaoutumia sasa.
Ukumbi huu wa sasa umejengwa kifahari, ambapo Mbunge akikaa kwenye sofa lake hata kama hajisikii usingizi atalazimika tu kulala kwa jinsi linavyobembeleza. Kuna taarifa kuwa ubunge huu uliogharimu mabilioni ya shilingi kujengwa, unataka kubomolewa ili uongezwe.

Ukiangalia Bunge la Kenya Ukumbi wao hauna tofauti na ule wa Karimjee, japo wao umepambwa zaidi. Lakini Wabunge wanakaa kwenye mabenchi tu. hata kama mtu unausingizi unaweza kushtuliwa na mwenzako. Lakini hii ya mheshimiwa kukaa kama yuko ofisini....


Waziri Steven Wassira akiuchapa usingizi



Mbunge wa Vunjo Augustine Mrema naye yuko ndotoni kabisa




John Komba ndiyo kabisa!







No comments:

Post a Comment