Monday, September 30, 2013

SERIKALI YAFUNGIA MWANANCHI & MTANZANIA

Dar es Salaam. Serikali jana ilitangaza kuyafungia magazeti ya Mwananchi na Mtanzania kuanzia Septemba 27, 2013 kwa kile ilichoeleza kuwa ni mwenendo wa magazeti hayo kuandika habari za uchochezi na uhasama. Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Habari (MAELEZO), Assah Mwambene ilisema gazeti la Mwananchi limefungiwa kwa siku 14 na gazeti la Mtanzania limefungiwa kwa siku 90. Magazeti hayo yamefungiwa kutokana na kuandika habari na makala zilizoelezwa zina nia ya kusababisha wananchi wakose imani kwa vyombo vya dola na kuhatarisha amani. “Gazeti la MWANANCHI limefungiwa kutochapishwa kwa siku kumi na nne(14) kuanzia 27 Septemba, 2013. Adhabu hii imetangazwa kwa Tangazo la Serikali(Government Notice )Namba 333 la tarehe 27 septemba,2013,” yasema taarifa hiyo. Kwa taarifa zaidi, tazama nakala ya tamko kamili la serikali juu ya kufungiwa kwa magazeti ya Mwananchi na Mtanzania hapo chini. TAMKO KAMILI LA SERIKALI Serikali imeyafungia kutochapishwa Magazeti ya MWANANCHI na MTANZANIA kuanzia 27 Septemba, 2013 kutokana na mwenendo wa magazeti hayo kuandika habari na makala za uchochezi na uhasama kwa nia ya kusababisha wananchi wakose imani kwa vyombo vya dola hivyo kuhatarisha amani na mshikamano ulipo nchini. Gazeti la MWANANCHI limefungiwa kutochapishwa kwa siku kumi na nne(14) kuanzia 27 Septemba, 2013.Adhabu hii imetangazwa kwa Tangazo la Serikali(Government Notice )Namba 333 la tarehe 27 Septemba, 2013. Gazeti la MWANANCHI limepewa adhabu hiyo kutokana na hivi karibuni kuchapisha habari zenye mwelekeo wa uchochezi na uvunjifu wa amani,mfano tarehe 17 Julai, 2013 katika toleo Namba 4774 ilichapisha habari isemayo “MISHAHARA MIPYA SERIKALINI 2013” kwa kuchapisha waraka uliozuiliwa kwa matumizi ya vyombo vya habari waraka huo ulikuwa wa Siri haukupaswa kuchapishwa Magazetini. Aidha, katika toleo la Jumamosi, tarehe 17 Agosti, 2013 lilichapisha habari yenye kichwa kisemacho “WAISLAM WASALI CHINI YA ULINZI MKALI” habari hiyo ilikolezwa na picha ya mbwa mkali mwenye hasira.Habari na picha hiyo ilitoa tafsiri ya kuwa Jeshi la Polisi lilipeleka Mbwa katika maeneo ya ibada ya waumini wa dini ya kiislam.Jambo ambalo halikuwa la ukweli. Jeshi la Polisi katika doria siku hiyo halikupeleka mbwa katika maeneo ya Misikiti.Serikali na jeshi la Polisi linaheshimu na kuzingatia maadili ya dini ya Kiislamu na kwa hiyo Jeshi lake haliwezi kupitisha au kuingiza mbwa katika maeneo ya ibada. Hivyo basi,kwa gazeti hili kuchapisha habari iliyokolezwa na picha ya mbwa ni uchochezi wa kulichonganisha Jeshi la Polisi na waumini wa dini ya kiislam mbwa ni najisi hapaswi kuingia katika maeneo ya ibada.

Saturday, August 31, 2013

Hearts broken as immigrants leave By Elias Msuya, The Citizen Correspondent With a major swoop by authorities planned any time following expiry of a presidential deadline for illegal immigrants to vacate, a number of them are living behind broken hearts and dwindling business fortunes among the locals. Ngara. Hundreds of families in Tanzania are pondering a bleak future owing to a big void created by the vacating masses of immigrants whose continued stay the government has described as untenable. With a major swoop by authorities planned any time following expiry of a presidential deadline for illegal immigrants to vacate, a number of them are living behind broken hearts and dwindling business fortunes among the locals. A week-long survey in the worst affected Kagera Region, reveals that the staggering movement of the illegal immigrants to mostly Burundi, Rwanda and Uganda is not without a share of whining from Tanzanians with intertwined family roots or deep business ties. Those who could not survive the purge are adeptly looking for means to beat the trap to continue with their lives even as local authorities give assurance of a more diplomatic recourse for genuinely separated families or investors. In many Ngara District villages, it is a story of mixed fortunes as the immigrants leave while locals are now forced to take measures to fill the socio-economic void. At the Rusumo border, village chairman Dauson Mhuru alias Kadende, is an unhappy man. Aged, 52, he is married to a Rwandese woman, Eluminata. Together, they have six children and raising another nine from the man’s earlier marriage which broke up. “I took this woman in the early 1990s and since then she has used a permit given by the Immigration offices. But now the government says she must leave the country, so how do I take care of my big family without her?” he asks. “I have gone to the Immigration offices and they have told me that her permit has expired and they have stopped issuing new ones. So now my wife must go to Rwanda and find a passport and seek Tanzanian citizenship, which will take a long time and will affect my family,” he added. Mhuru also added that he can’t go back to his first wife because they still have a matrimonial conflict. He said the family depended on income from a public toilet the wife was running at the border. “Despite my being the village chairman, I earn nothing because we don’t have a salary. I am just volunteering. I am engaged in petty trade and my wife supervises our public toilet project that brings in money to feed and educate our children, some of whom are in secondary school.” “They all need our material and moral support as their parents. The government should re think about its decision and spare families such misery, because this matter is affecting many families,” he adds. Mhuru said he was saddened by claims that as village leaders, they had been accepting bribes to allow in illegal immigrants. “I don’t speak for others but in my village, immigrants are those who came in the 70s most of whom are women,” he explained. The same predicament faces Sadiki Elias of Ruboma Village. He has a Burundian wife known as Elizabeth and a child. After President Kikwete issued the notice, his wife went to Burundi but came back after only a week, saying she needed medical care which was not available in Burundi. “I have lived with my wife for 10 years without a child but we got one last year. I have heard that people like her must leave the country but I need to take care of her and the child,” he said. Elias knows nothing about the dependent permit as they have lived without it all this long. “I will go for it anytime but we have been told nothing so far.” Another villager, Marko Lameck, also has a Burundian wife and seems ignorant of the paper work. “It’s true that my wife is Burundian and she left home after the government notice. But she is now back and she is at the farm,” he says urging the authorities to issue them with the said permits. Samuel Nkware, a Ngara resident says their local economy is likely to decline. “You know Burundians are muscular and work long hours as opposed to our own people. Many of us used them as labourers and for brick making. Most of the houses you see here were constructed by them.” Ms Jadida Mohamed, a garment dealer at Benaco suburb in Kasulo Ward, is also unhappy that most of her customers are leaving. “The immigrants, especially Rwandans who are pastoralists, are very rich and made our businesses thrive. I fear their departure means our businesses will dwindle,” she said. In Ngara town, Ms Maria Mugisha blames Tanzanian landlords and tycoons of bringing in the illegal immigrants to work in their farms and other businesses. Peter Nyabebda, who resides at Kumnazi Village near the closed refugee camps, says those who were repatriated during the closing of the camps are now loitering in the streets working as cheap labourers. “You know their countries are poor, they don’t have enough land and have no jobs, while while there’s enough land in our country; which is why they come here,” he said. However, the situation is different in Karagwe District. Aristides Muliro, who is a Bugene councillor, says illegal immigrants are problematic. He named one Njali Ndikukiko whose citizenship he claims is controversial but owns land at Nyakasimbe Ward. “They are problematic and because they are rich they are boastful and arrogant even when we tend to react to a problem involving them. He explained that Ndikukiko was rejected by villagers and later an official investigation found his residency wanting. “But the man is still around!” he exclaimed. Government response A senior Immigration officer at the Tanzania-Rwanda border at Rusumo, Mr Mahirande Samuel, says the law is clear on immigrations rules. “The law is clear and must be observed. Those married should have a dependent permit and renew them often. Those complaining do not observe these laws,” he says. He said their recent operation in Ngara township alone netted 268 Burundians, 52 Rwandans and two Ugandans. Ngara District commissioner Constantine Kanyasu says his district has more than 50,000 illegal immigrants. Some 10,000 have voluntarily gone back. “We have been educating our citizens on welcoming illegal immigrants as they take their budget share of social services such as education, health, water and economy,” he told The Citizen on Saturday. He said after an operation to mop those still holed up in Tanzania for a tune of Sh150 million, they will start a diplomatic move with the neighbouring countries to settle some marital and economic disputes.” Kagera regional commissioner Fabian Massawe says things will not be business as usual

Tuesday, July 2, 2013

OBAMA TANZANIA

Ziara ya Obama Ni ujio wa neema au mashindano ya rasilimali? Elias Msuya Wakati Rais wa Marekani, Barrack Obama akizuru nchini, kumekuwa na hisia tofauti miongoni mwa wachambuzi wa masuala ya maendeleo ya jamii na uchumi. Akizungumza baada ya kuwasili nchini, Rais Obama anasema kuwa ziara yake imelenga kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kwa maslahi ya Marekani na Afrika. “Tunachofanya ni kuongeza bidhaa tutakazozalisha na kuangalia vyanzo vya asili na vya kawaida. Ninachotaka kusema na nimekuwa nikisema katika ziara yangu Afrika, sasa tunaangalia si tu kutoa misaada bali kufanya ushirikiano wa kibiashara. Kila tunapotoa fedha au dawa ni muhimu tujenge miundombinu ya afya itakayosaidia Tanzania,” anasema Obama. Naye mwenyeji wake Rais Jakaya Kikwete akizungumza katika mahojiano maalum na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) ametetea ushirikiano kati ya Tanzania na Marekani akisema kuwa umesaidia kukuza uchumi wake na Afrika kwa ujumla. “Tunashirikiana na Marekani katika miradi mbalimbali na moja ya miradi mikubwa inagharimu kiasi cha dola 700 milioni. Kuna miradi mikubwa kama vile Pepfa inayogharimia mapambano ya malaria.” Akizungumzia ushindani kati ya mataifa ya Marekani na China katika miradi ya maendeleo nchini, Rais Kikwete anasema kuwa misaada ya Marekani imekuwepo hata kabla ya Rais wa China, Xi Jinping kuja Tanzania. “Kwa nini tuone kero kwa Waamerika au kwa nini Wachina wachukiwe kwa ushirikiano wao? Tunashirikiana nao katika nyanja tofauti. Tunafaidika kwa mambo mengi, kwanza tunaangalia misaada ya maendeleo kutoka Marekani, Japan, China, France, Ujerumani na popote pale. Vilevile tunaangalia uwekezaji na masoko ya bidhaa zetu,” anasema. Anaendelea kusisitiza ushirikiano na mataifa ya Asia, Ulaya na Marekani kwa lengo la kukuza uchumi. “Iwe Marekani kaskazini, kusini, Asia na kwingineko, ni ushirikiano tu. Ndiyo maana ukuaji wa uchumi wa Afrika unakua kwa kasi ya asilimia 6.6. ni uchumi unaokuwa kwa kasi ukifuatia bara la Asia.” Ushindani wa Marekani na China Ziara ya Obama imekuja ikiwa ni miezi michache tangu alipokuja Rais wa China, Xi Jingping ambaye naye alisaini mikataba 17 ya miradi ya maendeleo. Marekani yenyewe imewekeza katika miradi ya umeme ambapo kampuni ya Simbion inazalisha megawati 400 mkoani Mtwara na megawatt 100 Ubungo Dar es Salaam, huku kampuni ya Jacobson inazalisha megawati 200 Ubungo. Uwekezaji huo utasaidia kuongeza kiwango cha umeme kwani hadi sasa mahitaji ya umeme ni megawati 1100 na unaozalishwa ni megawati 675 tu, hivyo kupunguza tatizo la umeme linaloikabili asilimia 80 ya Watanzania. Kupitia mradi wa Millennia Challenge Corporation, Marekani imesaidia kutokomeza ugonjwa wa malaria visiwani Zanzibar katika mradi wake uliogharimu dola 698. Vilevile kuna miradi ya ujenzi wa barabara na chuo cha umeme kilichopo mkoani Morogoro. Lakini kila wanachofanya Marekani, China wanafanya kwa nguvu zaidi. China inajenga mradi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kuja Dar es Salaam utakaogharimu zaidi ya dola 1 bilioni. Mbali na miradi mingi ya ujenzi nchini, China pia wanajenga daraja la Kigamboni linalogharamiwa na Mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF). Kuna faida au hasara? Wakati mataifa ya Marekani na China yakishindana kuwekeza miradi ya maendeleo nchini, kumekuwa na mtazamo hasi na miradi hiyo huku wengine wakiona kuwa ni mbinu mpya ya mataifa hayo kupora rasilimali. Mhadhiri msaidizi wa Sayansi ya Siasa na utawala wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bashiru Ally anaona ushiriniano wa kasi na mataifa hayo ni kukua kwa itikadi kali ya soko huria duniani. “Zama za Dar es Salaam kuwa kitovu cha mapambano ya ukombozi Afrika zimekwisha eti kwa sababu nchi zote za Afrika ni huru. Wakubwa wa dunia (Marekani, nchi za BRICS na nchi za Umoja wa Ulaya) wanapishana kwenye viwanja vya ndege vya miji mikuu ya nchi za Afrika hasa zile zenye utajiri mkubwa wa raslimali,” anasema Bashiru na kuongeza: “Kinyang’anyiro cha ulimbikizaji wa mitaji na uporaji wa raslimali katika Afrika ni kikali sasa huenda kuliko kile cha enzi za ukoloni. Haishangazi kuona nchi za Afrika Kusini na Tazania zimekuwa na ugeni wa marais wa Marekani na China kwa kipindi kifupi sana.” Bashiru anasema ziara hizi zinafanyika huku vijana wa nchi hizo wakiwa katika mapambano makali na vyombo vya dola vya nchi hizo wakidai mambo mbalimbali yakiwemo mazingira mazuri ya kujikimu na elimu bora isiyo ya kibaguzi. “Hitashangaza ikiwa katika siku za usoni, Dar es Salaam itageuzwa na tabaka kandamizi kuwa Berlin ya Karne ya ishirini na moja. Sote tunaelewa yaliyoisibu dunia na bara la Afrika kutokana na maamuzi ya Berlin ya karne ya kumi na tisa. Afrika iliganywa vipande na kutawaliwa kikoloni kwa karne nzima,” anasema na kuongeza: “Wakati ule Waafrika hawakushiriki katika mikutano ya Berlin ya karne ya kumi na tisa. Waafrika wanaweza kualikwa kama wageni mashuhuri katika mikutano ya Berlin ya karne ya ishirini na moja ikiwa mkakati wa kuiuza Afrika kama bidhaa hautakomeshwa. Hata hivyo, mikutano ya kuligawa bara la Afrika tena itakuwa ya fujo maana wanaotaka kugawana raslimali za Afrika hawataafikiana kirahisi na kizazi cha sasa cha waafrika hakitasalimu amri.” Hata hivyo mawazo ya Bashiru yanapingwa na mwandishi wa habari mwandamizi wa gazeti la Jamhuri, Deodatus Balile alipokuwa akizungumza na Shirika la utangazji la Uingereza (BBC) akisema kuwa ni dhana potofu ya ujamaa na kujitegemea. “Kwa bahati mbaya sana, Watanzania tumelishwa dozi nzuri sana ya ujamaa na kujitegemea, lakini hatukufahamu vizuri maana yake. Kila unayeona ana simu mbili unadhani ni fisadi na kila unayeona ana nyumba mbili basi kakuibia wewe, si kweli,” anasema na kuongeza: “Kwenye uchumi kuna kutegemeana, kwamba huyu anazalisha pamba, huyu ana kiwanda cha kusokota nyuzi na huyu cha kuzalisha suruali, kwa jiyo mnategemeana. Tatizo kuna unyanyapaa, wakisikia Mmarekani wanajua haji hapa kwa wema, wanakumbuka matendo yake Iraqi, Afghanistan, Libya, wanadhani hayo ndiyo yanamleta Tanzania,” anasema Balile. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba anashauri nchi za Afrika kuwa na mkakati wa pamoja wa kulinda rasilimali zao. “Nchi za Afrika zenye bidhaa ghafi zingekuwa na utaratibu wa pamoja wa kujua namna gani tunaingia kwenye mazunguzo ya kuwa na mahusiano ya kibiashara na wenzetu tuweze kulinda maslahi ya nchi zetu,” anasema Profesa Lipumba. Wananchi wengi walikuwa na sahahuku ya kumwona Obama bila mafanikio. Wengi wameishia kumwona tu kwenye TV akihutunia.

OBAMA TANZANIA

Wananchi wengi walikuwa na sahahuku ya kumwona Obama bila mafanikio. Wengi wameishia kumwona tu kwenye TV akihutunia.

Friday, May 31, 2013

MATOKEO YA KITADO CHA SITA NA CHA NNE..

Matokeo ya kidato cha nne na kidato cha sita yatoka,yameongeza kwa asilima tisa.HONGERA KWA WOTE MLIFANYA VIZURI LAKINI POLENI PIA KWA WALE MLIFANYA VIBAYA kuna msemo unaosema "KIFELI MTIHANI SIO KUFELI MAISHA"bado unanafasi nzuri ya kufanikiwa katika maisha endapo utajituma huku ukimtanguliza MUNGU katika kila kitu unachokifanya sambamba na kutumia rasilimali zilizokuzunguka vizuri.ilikupata matokeo waweza kutembelea website hii www.necta.go.tz

Tuesday, May 28, 2013

"NGWAIR" msanii wa hip hop Tanzania afariki dunia

R.I.P Albet Mangwair •28 May 2013 Kiongozi wa kundi la cowboy mkali wa freestyle ambae alikua akiimba nyimbo za aina HIP HOP amefariki dunia huko nchini South Africa siku ya jumanne na mwili wake umehifadhiwa kwenye hospitali ya st.Hellen kwajili ya mipango ya mazishi.

Monday, May 6, 2013

MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI RUFIJI

Siri mgogoro wakulima, wafugaji Rufiji yabainika Naibu Waziri adaiwa kuchochea Elias Msuya Picha zikionyesha jamii za wafugaji wilayani Rufiji na mifugo yao. Nyingine ni Afisa Ardhi, Mifugo na Mazingira wa wilaya hiyo, Leo Rwegassira. Mgogoro kati ya wakulima na wafugaji wilayani Rufiji unaelezwa kusababishwa na kauli za viongozi wa Serikali huku viongozi wa wilaya hiyo na vijiji wakiwageuza wafugaji hao kuwa kitega uchumi kwa kuwadai rushwa. Mgogoro huo ulianza mara baada ya wafugaji waliokuwa katika bonde la Ihefu mkoani Mbeya kuhamishwa na wilaya ya Rufiji ikafanywa kuwa moja ya maeneo ya kufikia wafugaji hao. Mwezi Mei mwaka 2012 zilizuka vurugu katika kata ya Ikwiriri wilayani humo zilizosababisha watu kujeruhiwa na mali kuharibiwa ikiwa pamoja kuvunjwa kwa nyumba za wafugaji baada ya mkulima mmoja wa kijiji cha Muyuyu kudaiwa kuuawa na wafugaji. Wakizungumzia vurugu hizo katika ziara iliyofanywa na Shirika la kutetea wafugaji wa asili (Pingos Forum) wilayani humo hivi karibuni, baadhi ya wafugaji walimtuhumu Naibu Waziri wa Afya Dk Seif Rashid wakisema kuwa hotuba zake ziliwahamasisha wakulima kuwashambulia. “Vurugu zilianza baada ya baadhi ya wafugaji katika kijiji cha Muyuyu kudaiwa kulisha kwenye shamba la mkulima ambaye baadaye alifariki dunia. Lakini Mbunge alikuwa akihutubia mikutano na kuwaambia wakulima kuwa lazima watuondoe,” alisema Lago Laluka aliyevunjiwa nyumba. Naye Abdallah Nyalando aliyevunjiwa kiwanda cha kusindika maziwa alisisitiza madai hayo: “Ninao ushahidi wa video zikimwonyesha mbunge wetu akiwahamasisha wakulima kuwaondoa wafugaji kwenye maeneo yao,” alisema Nyalando. Hata hivyo Naibu Waziri Dk Seif Rashid amekanusha madai hayo akisema alikuwa akitekeleza uamuzi wa Baraza la Madiwani la wilaya hiyo. “Unajua mtu anaweza kusema lolote, hata hapa tunapozungumza unaweza kuyatafsiri maneno yangu unavyotaka. Nilichokisema mimi ni kuhusu uamuzi wa Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Rufiji kwamba bonde hilo litumike kwa ajili ya kilimo siyo mifugo. Lengo ni kulitunza na uharibifu wa mazingira. Siyo Dk Seif kasema ni Halmashauri,” alisema Dk Rashid. Dk Rashid ambaye ni mbunge wa Rufiji amesisitiza kuwa eneo hilo siyo la wafugaji. “Hilo tatizo liko nchi nzima na hata kabla sijawa Mbunge nililifahamu na nilipokwenda Bungeni nilimuuliza Waziri wa Mifugo akanijibu kuwa eneo hilo siyo la wafugaji bali ni la kilimo tu,” alisema. Akizungumzia uamuzi wa Mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza aliyeagiza kuwa wafugaji hao wasiondolewe hadi watakapopatiwa maeneo mengine, alisema kauli hiyo si lolote kama haifuati sheria ya mwaka 1975. “Agizo la mkuu wa mkoa linapaswa kwenda na sheria ya mwaka 1975 inayotaka bonde hilo liwe la kilimo na Waziri alishajibu hivyo,” alisisitiza Dk Rashid. Dk Rashid amedaiwa kutoa kauli za kuwachochea wakulima kuwaondoa wafugaji hao kwa madai ya kuingilia mashamba ya wakulima siku chache kabla ya kutokea vurugu hizo. Baadhi ya wakulima wa Ikwiriri wilayani humo wameilaumu Serikali kwa kutowaelekeza wakulima kwenye maeneo waliyopangiwa. “Serikali ndiyo imewaelekeza wakulima kuja hapa Rufiji na kila siku wanachukua fedha za vibali lakini wameshindwa kuwapeleka kwenye maeneo yao,” alisema Juma Ngwele. Naye Mwajuma Mwinyikambi aliwalaumu wafugaji kwa kulisha mifugo yao kwenye mashamba ya watu. “Tangu wamekuja hao wafugaji hapa amani imepotea kabisa, kwa kweli hatuwataki. Ni kweli tunapata maziwa na nyama kwa urahisi lakini ni wakorofi, wanaharibu mazao yetu kila mara,” alilalamika Mwajuma. Kauli ya mkuu wa mkoa Akizungumzia suala hilo, Mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza alisema agizo lake lilikuwa ni wakulima kwenda kwenye maeneo waliyopangiwa na siyo vinginevyo. “Agizo langu lilikuwa ni la mpango kazi. Mwaka 2008 wakati Serikali inawahamisha wafugaji kutoka bonde la Ihefu, wilaya ya Rufiji ilikuwa ni moja ya maeneo waliyotakiwa kufikia…Nilichoagiza ni wakulima kwenda kwenye maeneo waliyopangiwa, siyo vinginevyo,” alisema Mahiza na kuongeza: “Wafugaji waliokwenda kwenye maeneo yao waliyopangiwa, tumewaacha, ila wale walio kwenye maeneo yasiyoruhusiwa waondoke.” Serikali haikujiandaa? Akizungumzia kero za wafugaji wilayani humo, Afisa ardhi, maliasili na mazingira, Leo Rwegasira amekiri kwamba Serikali haikuwa imeandaa maeneo ya kuwaweka wafugaji baada ya kuhamishwa kutoka bonde la Ihefu. “Kabla ya kuja wafugaji hawa hapa Rufiji palikuwa shwari, lakini walipokuja mwaka 2007 imekuwa ni vurugu tupu. Awali tuliambiwa kuwa kuna mifugo itakayobaki hapa, mingine itakwenda Lindi na Mtwara hivyo maeneo yaandaliwe. Lakini hadi wanafika hakukuwa na maeneo ya kuwaweka na hakukuwa na fedha za kuainisha maeneo hayo,” alisema Rwegasira. Kutokana na hali hiyo alisema kuwa walitenga vijiji tisa ambavyo waliainisha maeneo ya wafugaji haraka haraka. “Wafugaji wengi walipokuja walifikia kijiji cha Muyuyu kando yam to Rufiji, hata wale waliotakiwa kwenda Lindi na Mtwara wakaishia kando yam to huo,” alisema. Akizungumzia uwezo wa eneo hilo kuchukua mifugo alisema kuna hekta 7874 zenye uwezo wa kuchukua mifugo 39,362 lakini hadi sasa kuna mifugo 109,239. “Hadi sasa tumetenga vijiji 39 ili tuainishe maeneo ya wafugaji na zinatakiwa sh81 milioni na kati ya hizo Halmashauri imetenga sh10 milioni. Ndiyo maana tumewaambia wafugaji nao wachangie sh170, 000 kila mmoja, lakini hawataki, ndiyo maama mgogoro hauishi,” alisema. Akizungumzia kampuni ya Mkiu Poultry farm iliyopewa eneo la uwekezaji badala ya wafugaji wa ng’ombe, Rwegasira alisema huo ulikuwa ni uamuzi wa vijiji hivyo na walipata kibali cha kamishna wa ardhi. Hata hivyo Waziri wa Maendeleo ya mifugo na uvuvi Dk David Mathayo amekanusha kuwa Serikali ilikurupuka kuwahamisha wafugaji hao. Dk Mathayo amekwenda mbali zaidi na kusema kuwa Tume ya matumizi bora ya ardhi inayoshirikisha wizara za Maliasili na Utalii, Mifugo na uvuvi na wizara ya ardhi inaendelea na upimaji wa maeneo ya wafugaji wanaohamishwa. “Kila Halmashauri ina utaratibu wake siwezi kuingilia, lakini kunaTume ya matumizi bora ya ardhi inayohusisha wizara za Maliasili na utalii, Mifugo na Uvuvi na wizara ya Maji inayoainisha maeneo ya wafugaji,” alisema Dk Mathayo na kuongeza: “Tumetenga kiasi cha sh1.2 trilioni kwa ajili ya kazi hiyo iliyoanza miaka mitatu iliyopita. Tumeshapima mikoa 19 kutoa Dar es Salaam, wilaya 66 na vijiji 445. Mwisho wa kazi hii utategemea upatikanaji wa fedha.” Rushwa yatawala Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili wilayani humo umebainisha kuwa Serikali haikuwa imetayarisha eneo maalum la kuwahamishia wafugaji hao hali inayowafanya wasumbuliwe na viongozi wa vijiji wanaowadau fedha ili wawape waeneo ya kulisha mifugo hiyo. Mmoja wa wafugaji hao kutoka kijiji cha Muyuyu, Mbuga Pawa alisema kuwa tangu walipofika wilayani humo wamekuwa wakilipia fedha za usajili kila unapokuja uongozi mpya. “Mara ya kwanza tulipokuja tulilipia vibali vya kukaa vijiji kwa sh30,000, baadaye tukaambiwa siyo halali, tukasajiliwa tena kwa vibali vingine kwa sh80,000 na wengine sasa wanasajiliwa kwa sh100,000. Hadi sasa hatujui hasa ada ya kusajiliwa ili tupewe maeneo ni shilingi ngapi,” alisema Pawa. Naye Joseph Bangi, mfugaji katika kijiji cha Nyamisati anasema mara kwa mara amekuwa akifuatwa na viongozi wa kijiji wakimsumbua na kumdai fedha. “Nilihamia hapa kutoka bonde la Ihefu mwaka 2006 nikalipishwa sh150,000 kama ada ya kufikiriwa na kijiji. Mwaka 2007 nikalipishwa tena sh150,000 na mwaka huu nimelipishwa sh50,000, nimeshatoa sh40,000. Ilimradi kila siku ni kufuatwafuatwa tu, ukilipa kibali hiki kesho unaambiwa siyo halali, unalipa tena,” anasema Bangi. Wafugaji wengine wa jamii ya mang’ati, Saleh Chafuchafu, Masharubu Chafuchafu na Masauda Chafuchafu wanalalamika kufukuzwa katika vijiji vya Kilimani A na B licha ya kuishi tangu mwaka 2006. Mbali na malalamiko ya rushwa, mwezi Aprili mwaka huu, Saleh Chafuchafu amejikuta akilimwa faini ya sh4,080,000 kwa kile kinachodaiwa kuwa mifugo yake iliingilia shamba la mtu. Akizungumzia tuhuma hizo, Afisa mtendaji wa kata ya Ngorongo Uwesu Mbembeni amekiri kuwepo kwa vitendo vya rushwa huku akimtaja aliyekuwa Mwenyekiti wa kijiji cha Ngorongo Magharibi Hassan Mpange kuwa alikusanya kiasi cha sh665,000 kwa wafugaji akidai ni ada ya kuwajadili ili waruhusiwe kuishi na mifugo yao. “Ni kweli kuna mwenyekiti wa zamani wa kijiji cha Ngorongo alichukua sh665,000 za wafugaji 19 akisema ni ada ya kijiji kuwajadili. Lakini fedha hizo hazikufika katika serikali ya kijiji. Mimi nilimwita ofisini kwangu nikamwambia awe tayari kwenda mahakamani,” alisema Mbembeni. Juhudi za kumpata Hassan Mpange kujibu tuhuma hizo hazikufanikiwa kutokana na kukata simu kila anapopigiwa. Akizungumzia eneo walilofikia wafugaji hao ambalo sasa wamefukuzwa na kupewa mwekezaji (Mkiu Poultry Farm) anayelitumia kufugia kuku, Mbembeni alisema: “Ni kweli wafugaji walitangulia katika eneo hilo lakini hawakuwa na vibali halali vya kuishi hapo na mkuu wa wilaya aliafiki kwamba waondolewe.” Amebainisha kuwa mwekezaji huyo alipewa eneo la vijiji vya Ngorongo Magharibi na Mashariki lenye hekta 2026 na kuwaacha wafugaji waliolipia hela zao solemba. Hata hivyo alisema kuwa Mkuu wa mkoa wa Pwani alikataza wafugaji hao kusumbuliwa hadi litakapotafutwa eneo jingine. Kwa upande wake Mwenyekiti wa kijiji cha Ngorongo Magharibi Mohamed Mkwega amekiri kuchukua fedha za wafugaji hao akidai ni ada ya uvamizi na posho za kikao. Katika risiti za malipo hayo (nakala tunazo) zilizotolewa Februari 11 mwaka huu, Mwenyekiti huyo alikusanya kiasi cha sh1.8 milioni kutoka kwa wafugaji akidai ni ada ya kikao cha kuwajadili. “Ni kweli tulichukua fedha hizo, ndiyo utaratibu wa kijiji chetu wala siyo utapeli. Fedha hizo zimetumika kama posho za vikao vya kuwajadili kwani kila mjumbe hulipwa sh2000,” alisema Mkwega. Hata hivyo alikiri kuwepo kwa vitendo vya rushwa na kwamba kuan wakati viongozi wa vijiji hutoa hati feki kwa wafugaji. Naye afisa mtendaji wa kijiji hicho, Juma Kilalile alisema tatizo la wafugaji katika vijiji hivyo kuzidiwa na idadi ya mifugo. “Tulifanya sensa ya mifugo tukakuta kuwa kuna zaidi ya ng’ombe 6,000 wakati uwezo wetu ni ng’ombe 130 tu,” alisema. Takukuru Rufiji Akizungumzia malalamiko hayo ya rushwa, Afisa wa Taasisi ya kupamabana na kuzuia rushwa (Takukuru) wilayani Rufiji, Saada Mzimba amekiri kuyapata malalamiko ya rushwa kutoka kwa wafugaji na kwamba tayari kuna kesi mbili baada ya malalamikio hayo. “Ni kweli tunapata malalamiko hayo, kwa mfano kuna wafugaji kutoka kijiji cha Mkongo walifika hapa kulalamika. Huwa tunauliza kama wamepata vibali vya kuishi vijiji hivyo, maana wengine wanavamia tu.,” alisema na kuongeza: “Hadi sasa tuna kesi mbili tumewafungulia viongozi wa vijiji wanaodai rushwa. Vilevile tunawashauri waende kwenye maeneo waliyoandaliwa badala ya kutangatanga.”